Thursday, December 17, 2009

HUYU NDIYO NYOTA!

JAMILA (Latifa Idabu)
Aling'ara kwenye filamu ya Sanda Nyeusi


Kafunika kwenye ASALI CHACHU


Cheki hili pozi, hafi mtu kweli hapa?!



HAIFANANISHIKI!

ASALI CHACHU!
ASALI CHACHU ni filamu ambayo huwezi kuifananisha na yeyote kati ya ambazo umewahi kuziona katika maisha ya filamu za kibongo.
ASALI CHACHU ni filamu daraja kati ya filamu za burudani na filamu za kuelimisha, unaelimuka huku ukiburudika.

ASALI CHACHU ni filamu ambayo unaweza kuiangalia na familia yako, haijatengenezwa na wale wanaoamini kuwa kuacha vichupi nje ndiyo filamu inauza.

Friday, November 20, 2009

Binti wa Kiislam!



Anaitwa Wema binti Sepetu, ni binti wa kiislamu, mtanashati asiye na makuu na mmojawapo wa waigizaji wakali katika tasnia la filamu Tanzania. Kama unajua vingine, KIMPANGO WAKO!

Hili Movie linakuja!


Filamu hii, ndani yuko Thea, Christian Bella (Rais wa Masauti) na wengine kibao. Inaitwa 'Hisia Zangu'.

Saturday, November 14, 2009

MKOREA wa Filamu Tz!


Huyu anaitwa Park Doeng I, raia wa Korea ambaye amejitolea kuwasaidia wadau wa filamu Tanzania ili zipatikane filamu zenye ubora na viwango vya kimataifa, na ameanza na kikundi cha Safari Arts cha NIT, Dar. Hapa anaonyesha udugu kwa kum'beba mtoto wa kiswahili, tena mgongoni. Umeiona saa ya huyo mtoto?

Monday, November 9, 2009

Mtanashati!

Wako ambao tumewazoea kwa utanashati, mfano ni huyu bro anaitwa Tino. Lakini sasa kila muigizaji wa kiume anajitahidi kwa 'mapouda' akiigiza muvi. Tunajua kuwa filamu ni kwa ajili ya kuonyesha maisha asilia, je katika uhalisia wanaume wa kibongo ni watu wa mapouda?

Anti Ezekiel

Mkali wa muvi za kibongo, Anti Ezekiel Greyson 'Jujuman' (Binti wa winga teleza wa Simba S. C. enzi miaka ya themanini)Mauzo yapo?

Tuesday, October 20, 2009

A KOMANDO YOSSO film!

Hapa wanacheza Mnanda!

Hapa wako Maskani, wamewachenjia wenzao


Hapa Mkwere kajipindua, eti anawauzia kahawa!


COMMANDO YOSSO Xclusive!


Kuveta na Komando Yosso wakiwadhibiti Sungusungu! Hii ni katika filamu ya Komando Yosso

Monday, October 12, 2009

DUDE wa BONGO DSM

Hapa alikuwa akiigiza katika filamu ya 'MACHO MEKUNDU'

Long time baba'ake

This was during the production of a film 'Miss Bongo'
Kwa sasa Mtitu (aliyekaa), kafungua ofisi ya kufa mtu maeneo ya magomeni inayojishughulisha na utengenezaji na usambazaji wa filamu.
Bravo Brother!

Friday, October 9, 2009

Kitimtim!

Kiwewe, Matumaini na Mtanga katika filamu ya MBWEMBWE

Ni utumwa wa akili?

Warembo wa bongo a.k.a Mamiss wakimuenzi mfalme wa muziki wa pop wa Marekani, Michael Jackson katika shindano la Vodacom Miss Tanzania.
Si bora wangemuenzi Nasma Khamis kwa 'kurusha roho'!

Friday, October 2, 2009

Nyumbani ni Nyumbani!

Mdau 'Sammy Classic' akiwa na bibi zake Upareni

Thursday, September 17, 2009

JULIUS KAMBARAGE NYERERE


Suala sio tu kumkumbuka mzee huyu, wote tunamkumbuka. Tunamkumbukaje? hilo ndilo haswa tunalotakiwa kujiuliza katika nafsi zetu.
Wengi wanajidai kumfuata ili tu wapate muonekano mzuri mbele ya jamii ya watanzania, lakini moyoni mna yenu machafu!
Kama kweli mnamkumbuka hebu testini kurudisha
AZIMIO LA ARUSHA!

Ze Telefoni!


Katika filamu ya Mbwembwe ya Kiwewe na Matumaini, utapata zis telefoni

Itifaki Imezingatiwa!!!

Kiapo hapa kinaliwa na Mzee mzima Kingunge!

Wednesday, September 16, 2009

Changamoto

Ni sawa kudai haki yako, lakini unajua namna na wapi pa kuidai? hapa ndipo suala la shule linapokuja. Wasanii tutafute elimu!
Harakati za kudai haki bila kutumia akili ni sawa na kutaka kuzuia maji kwa godoro.

Friday, September 4, 2009

SWAHILIWOOD

Kamati teule ya kuanzisha Swahiliwood

Baadhi ya wajumbe wa Bodi ya filamu wakiwa na wadau


Wadau wakifuatilia mchakato

Friday, August 28, 2009

‘FLASHBACK’ KATIKA FILAMU

Dhumuni la flashback katika filamu ni kumpa mtazamaji maelezo yanayohitajika katika kuifanya hadithi iendelee vizuri ama kutoa ufafanuzi wa matendo yanayofanywa na mhusika katika filamu.
Flashback inatakiwa kutumiwa pale tu kwenye ulazima wa kufanya hivyo, inatakiwa iwe ya tukio la kipekee ambalo linasherehesha kitendo anachokifanya mhusika kwa wakati huo.
Tukio hilo unaloliweka katika flashback lazima limfanye mtazamaji aelewe kuwa ndilo linalomsukuma mhusika atende kitendo akitendacho kwa muda huu.

HAPO VIPI?


MADIKODIKO!

Hii ni katika filamu ya 'MBWEMBWE'

WEWEEEEEEEE!

Usipimie hicho kichapo kwa staili hii hapa!

Saturday, August 8, 2009

JIELIMISHE!

Japo wanadai kuwa mada za mapenzi zinauza lakini naamini kuwa wanachoandika wasanii ama kuongelea ndio mwisho wa upeo wao wa uelewa.
Badala ya kutoa ujumbe watu wanashindana kuwaacha uchi waigizaji wa kike huku wenyewe wakishindana katika kuazima mavazi na magari ya kifahari.
Dhana hiyo ndiyo iliyopelekea baadhi ya wadau wa filamu kuwaambia wasanii wa kike wasiokuwa maarufu kwa kukaa uchi kuwa hawana mvuto! Ujinga huu.
Wanashindwa kuelewa kuwa wateja wao wakubwa ni kina mama na watoto, sasa unapomuonyesha mama yako au mdogo wako kichupi cha muigizaji wako wa kike ndio ubunifu?
Ili uweze kuelimisha jamii ni lazima kwanza ujielimishe mwenyewe!

Dah!

Mzee Magali katika A Girl from Nigeria!

Monday, August 3, 2009

UNALIA NJAA!!!!

Kuna wastani wa filamu tano ambazo huingizwa sokoni kila mwezi, haya ni makadirio yanayotokana na filamu ambazo hutangazwa sana na vyombo vya habari.
Lakini katika uhalisia, ni kwamba kuna kati ya filamu saba hadi kumi zinazoingizwa sokoni kila mwezi.
Katika mkutano mmoja wa wadau wa filamu uliofanyika hivi karibuni kuna mdau alitoa tathmini kuwa kuna zaidi ya maktaba laki moja zinazowakodisha filamu wananchi, na zote hizo zina wastani wa nakala halisi tatu tatu. Hizo ni mbali ya zinazonunuliwa kwa ajili ya kuangaliwa majumbani.
Tanzania ina watu takribani milioni arobaini, chukulia kuwa wateja wa filamu ni asilimia tano tu, basi hapo zitahitajika nakala milioni mbili.
Ukiongea na wasambazaji watakwambia kuwa filamu yenye mafanikio kuliko zote haijafikia nakala elfu hamsini! Ila kawaida nakala zinazotolewa hazifiki elfu kumi. Hazitoshi hata kusambazwa kwenye maktaba!
Hebu fikiria sasa, endapo filamu zinatoka nakala japo hizo laki tatu tu za kutosha maktaba, na bei ya nakala moja iwe ni shilingi elfu tatu.
Faida ikiwa mia tano tu, kila muvi mdau unapata milioni 150! Njaa itakuwepo?

FULL KUUZA!


Dennis 'akiuza nyago' filamuni

WA UKWELI?

Binti Sepetu, ni mkali ile mbaya filamuni na umissini. Kwingine? Sijui!

INAKUWAJE PALE?


Hapa wanaume kazini!

SWAHIBAAA!

Hapa ndio Richie anaingia na mzigo wake, Rose Ndauka huku 'Simba' JB akipata Kiroba. YAAN FULL MZUKA!

Hili ni pozi tu la 'kuuzia nyago'

Hapa 'Simba' JB naye analilipa pozi la Richie
Hawa jamaa USIWAPIMIE


WARSHA YA FILAMU MORO

Kundi la Mtazamo African Theatre limeandaa warsha ya uandishi na uandaaji wa filamu itakayofanyika katika hoteli ya MASUKA Village, Morogoro mwisho wa mwezi huu.
Warsha hiyo itaendeshwa na wataalamu toka Daraja Project, mradi wa filamu ulio chini ya taasisi ya Movie n' Style Tanzania.

BINTI KIZIWI AWA MISS KOROSHO TZ

Hii ni habari toka Morogoro ambapo Caroline ambaye ni kiziwi ameibuka kuwa Miss Korosho Tz baada ya kuwafunika mbaya vidosho wengine 11 Jumamosi 1/8/09 katika NANENANE Fashion week!

Saturday, August 1, 2009

HAPO VIPI?

Haji Adam akiwa na kimwana katika muvi inayokwenda kwa jina la Quick Money
Hapa Richa Adhia akiwa na kidume katika muvi inayoitwa Full Moon


Wednesday, July 22, 2009

Filamu MORO wamegoma!

Wadau wa filamu wa Morogoro hasa wasanii, wamegoma kuendelea kutumika na watengeneza filamu wa kutoka Dar kwa kucheza vipande vichache tu, sasa na wao wanataka kutengeneza za kwao ili wa Dar nao wacheze vipande vichache.

Jamal kutoka kundi la MTAZAMO la hapa mji kasoro bahari yuko Dar akifanya maongezi na taasisi ya Movie n' Style Tanzania (MSTZ) kuangalia uwezekano wa kuanza kuangusha maMuvi toka milima ya Uluguru!
KAENI CHONJO

MISS KOROSHO TANZANIA

Khabar ndo hiyo yakhe!
Kama unadhani umeshasikia kuhusu mashindano yote ya U-miss hapa Bongo, utakuwa umechemka.
Huku Morogoro kuna dude linadondoshwa linaitwa...
MISS KOROSHO TANZANIA
Ukitaka kujua vigezo na nani atatangazwa basi fika Hotel Oasis siku ya tarehe 1/8/2009.

Tuesday, July 21, 2009

KIPROFESHENO ZAIDI!

DARAJA PROJECT
We bring in Professionalism in filmmaking Tanzania
Wanaprofenisha muvi za kibongo, wanatoa huduma kwa gharama zinazoendana na hali halisi ya soko la Tanzania.
Scriptwriting, Directing, Production Management & Production Crew.
Wako 5th Floor MAVUNO HOUSE, Azikiwe Street, Dar es Salaam. Simu: o22 2125544 au 0784 235444

Mitindo Uluguruni!

Bonge la shoo la mitindo linatarajiwa kudondoshwa tarehe 1/8/2009 katika ukumbi wa Hotel Oasis, Morogoro kuanzia saa 2 usiku. Shoo hilo limepewa jina la.....

NANE NANE FASHION WEEK

Na linadondoshwa Mji Kasoro Bahari na Nepa Promotion chini Alex Nikitas. Itakuwa nomaaa!

Monday, July 20, 2009

Wa Filamu mpo?

Katika hotuba nzima iliyotolewa bungeni na Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo, kinachohusu filamu ni hiki:

Bodi ya Filamu na Michezo ya Kuigiza
66. Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha mwaka wa fedha wa 2009/10 Bodi ya Filamu na Michezo ya Kuigiza itatekeleza yafuatayo:
  • Kukagua na kupanga katika madaraja filamu 500 (Video, DVD, VCD na VHS) na kutoa vibali.
  • Kuandaa na kukamilisha mchakato wa kuandika kanuni za utekelezaji wa sheria Na. 4 ya mwaka 1976 ili zitangazwe na kusambazwa.
  • Kukusanya taarifa na takwimu za kumbi za sinema na michezo ya kuigiza ili kuzipanga katika madaraja. Kupitia na kuhakiki miswada ya utengenezaji wa filamu na kutoa vibali.
  • Kuhamasisha jamii na kutoa elimu kwa wadau 250 kuhusu kulinda, kuendeleza utamaduni, maadili na ujumi wa watanzania katika filamu na michezo ya kuigiza.

Mfuko wa Utamaduni (69 kipengele cha nne).

  • Kuwajengea uwezo na kuweka tarifa (capacity building and mapping) za watengeneza filamu wanaoinukia.

MNATEGEMEA NINI?

Saturday, July 18, 2009

Eti huyu kawa Afande..

Katika msako wa kumtafuta KUVETA, huyu jamaa alikuwa front kama Ditektive Lawrence. Hilo ni muvi moja hivi la 5 Effect ambalo wamekamua mastaa kibao, Big, Baba Haji, Mashaka, Bi Hindu, Kingwendu, Mkwere, Mzee Korongo, Mzee Msisi wa Msisiri na wengine kibao tu. SIJUI WATALIITAJE MUVI HILO kwa kuwa jina lake la awali (jina kapuni) kuna watu washaliigizia.

LINI TENA?

Mh. Bendera, Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo akitoa Tuzo ya filamu bora kwa mwaka 2008.
Mzee Bawji, Wakurugenzi Octa na Galus wakiwa na Richard wa BBA II na Kanumba 'the Great'


Anko Richie wa UDSM akimtuza Emanuel (Kulia) huku Kanumba akishuhudia


Regina Dundelova (Kulia) wa EU Film Festival 08 akiwa kwenye Vinara 08


Jaji Cuthbert Kabunga (Kushoto) toka CMK Production akimkabidhi Tuzo Mpiga Picha bora, Rashid Mrutu